Mbeya Institute Of Journalism (MIJO) inakukaribisha katika mwaka wa masomo wa Februari hadi Desemba 2010



Serikali ya Wanafunzi ya Chuo (SOMIJO) inakukaribisha kwa moyo mkunjufu katika tasnia hii ya Uandishi wa Habari zilizojawa na ukweli zenye kuleta maendeleo kwa mwananchi husika na taifa kwa ujumla.

Saturday, November 13, 2010

SU KYI AACHIWA HURU


KUTOKA CHUMBA CHA HABARI

Kiongozi wa upinzani nchini Myanmar, Aung San Suu Kyi ameachiwa huru leo na uongozi wa kijeshi wa nchi hiyo.

Uongozi wa kijeshi nchini Myanmar umemuachia huru kiongozi wa upinzani nchini humo, Aung San Suu Kyi. Magari maalum leo yaliwasili katika nyumba ya kiongozi huyo iliyoko pembezoni mwa ziwa na polisi waliondoa vizuizi pamoja na senyenge.
Suu Kyi aliusalimia umati wa wafuasi wake wapatao 1,000 ambao walikuwa wamekusanyika katika lango la kuingilia kwenye nyumba hiyo. Mshindi huyo wa Tuzo ya Amani ya Nobel, ametumikia kifungo cha nyumbani kwa takriban miaka 21.
Kitendo cha kuachiwa kwa mtetezi huyo wa demokrasia kimepongezwa na viongozi mbalimbali wa Ulaya, Marekani na Jumuiya ya mataifa ya Kusini-Mashariki mwa Asia-ASEAN.
Kifungo hicho cha nyumbani dhidi ya Suu Kyi kimemalizika ikiwa ni wiki moja baada ya vyama vinavyoungwa mkono na uongozi wa kijeshi wa Myanmar kushinda katika uchaguzi ambao mataifa ya Magharibi yameuelezea kama wa uzandiki.

Imeandikwa na: Grace Kabogo (AFP, DPA)

MBOWE KIONGOZI KAMBI YA UPINZANI BUNGENI

KUTOKA CHUMBA CHA HABARI
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimemteua mbunge wa Hai, Freman Mbowe kuwa kiongozi wa kambi ya upinzani katika bunge la 10 la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mbali na kuteuliwa kwa mbunge huyo pia chama hicho kimemteua mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto kuwa makamu wa kambi hiyo bungeni.Hata hivyo uteuzi huo umefanya kambi ya upinzani bungeni kumeguka kwa vyama vingine kutokubaliana na uteuzi huo, na kudaiwa kuundwa kambi mbili za upinzani.Awali Mbunge wa Wawi (CUF), Hamad Rashid Mohamed, ndiye alikuwa kiongozi mkuu wa usemaji kambi ya upinzani na Aliyekuwa mbunge wa Karatu, Wilbrod Slaa alikuwa naibu wake.


Imeandikwa na :Johnson Jabir

Saturday, November 6, 2010

Agatha Mboya

ZAIDI ya Sh 50 billioni zitatumika katika kukamilisha mradi mkubwawa maji unaojengwa katika Jiji la Mbeya.

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka (Uwasa) katika Jiji laMbeya, Simion Shauri alisema mradi huo ulioanza kujengwa Septemba2008 unatarajia kukamilika mwakani na kwamba utawezesha wakazi wote wajiji hilo kupata maji safi na salama katika kipindi chote cha mwaka.

Shauri alisema fedha za ujenzi wa mradi huo wa maji zimetolewa naShirika la Kijerumani KFW pamoja na Umoja wa Nchi za Ulaya (EU) kwakushirikiana na Benki ya Dunia.Kwa mujibu wa maelezo ya Shauri kukamilika kwa mradi huo wa majikutaongeza kiasi cha maji kutoka wastani wa mita 32,000 kwa siku zasasa hadi kufikia mita za ujazo 49,000 kwa siku.

Aliongeza kusema kuwa chini ya mradi huo mkandarasi kutoka nchini UfaransaSogea Satom anajenga mitambo ya kisasa yenye uwezo mkubwa wa kusukumamaji katika vyanzo vya Nkwanana Mwatezi, na LunjiMkandarasi huyo pia anajenga mitambo ya kisasa ya kutibia maji katikavyanzo vya Meta Sisimba, Sai, Lunji, Mwatezi, Iduda na Nsalagapamoja na kujenga vituo vipya vya kusukuma maji katika eneo la SwayaNelotia, Nsalaga na ImetaAlisema matanki saba makubwa ya kuhifadhia maji yanajengwa katikamaeneo ya Veta, Forest mpya, Iwambi, Imeta, Iganjo, Nsoho, na Iduda.

“Mradi huo pia unaongeza mtandao wa maji kwa kuunganisha na mabombayenye urefu wa kilomita zaidi ya 37 na kujenga viungo kwa wateja wapyana kupanua mabwawa ya kutibu maji taka katika eneo la Kalobe ilikuepusha magonjwa ya milipuko kwa wakazi wanaoishi katika maeneohayo,”alisema.

Alisema fedha hizo pia zitatumika katika kununua vitendea kazi kwaajili ya matengezo ya mtandao wa mabomba na shughuli za umeme namagari matatu ya maji taka pamoja na ujenzi wa vyoo mashuleni naujenzi wa vyumba vya kuishi watumishi na ujenzi karakana za kupimausahihi wa dira za maji.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo wa Mamlaka ya Maji safi na Majitakajijini Mbeya, utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 80 na zaidiya jumla ya Sh 27 bilioni zimekwishalipwa na gharama za kutekelezamradi mzima ni zaidi ya Sh 56 milioni. Awamu ya pili ya ujenziitagharimu Sh 13 bilioni.

JIJI LA MBEYA LAKABILIWA NA UKATA WA MAGARI YA TAKA

Na Onesmo Alfred.

LICHA ya mkoa wa mbeya kuwa jiji lakini bado unakabiliwa na uhaba mkubwa wa magari ya kubeabea takataka jijini hapa .

Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana baadhi ya wakazi wa maaeneo ya Mwanjelwa na Soweto wamesema hali hiyo imekuwa ikiwafanya wao kuwapa kikwazo kutokana na hali ya baadhi ya maghuba kujaa taakataka na nyigine kumwangwa nje.

“Mimi hali hii inanikera sana kwasababu husababisha biashara yangu kwenda vibaya kutokana na wateja wangu kukimbia kutokana na ghuba hili kujaa taka na kutoa harufu kali pia kutokana na biashara yangu ya mamalishe nina somesha watoto watatu wakiwemo wa sekondari wawili na wa shule ya msingi mmoja hivyo kukosa wateja kwangu hunisababishia kukosa ada ya watoto wangu, ”alisema.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jiji la mbeya Juma Idd alisema halmashauri ilikuwa ikikabiliwa na uhaba mkubwa wa magari yakubebea takataka.

Idd alisema hivi sasa halmashauri iko kwenye mikakati yakununua magari ilikuweza kukabiliana na hali hiyo ilikuweza kuufanya mkoa wa mbeya kuwa nahadhi ya jiji na kuwa halmashauri ina mpango wa wakuwa na gari kumi na sita haya niya side roder(yakubebae takataka) na skip master

Alisema halmashauri ilikuwa na magari matatu yakubebea takataka (side roder) likiwepo moja kwaajili ya kubebea maghuba (skip master) ilikuweza kukabiliana na hali hiyo ya kero ya takataka hizo.

Ambapo amesema jiji lina uwezo wakuzalisha tani 1260 kwa siku hivyo gari moja lina uwezo wakubebe safari tatu ambazo ni sawa na tani 14 kwa siku halmashauri ina uwezo wakubeba tani 420 kwa siku

Mkurugenzi alizitaja baadhi ya sababu ambazo husababisha uzalishaji huo wataka kuwa ni idadi kubwa ya watu katika jiji la mbeya likemo lilela kushamili kwa biashara katika jiji la mbeya.

Aidha alisema kuwa jiji la mbeya linashika nafasi ya tatu kwabiashara kitaifa hivyonilahisi sana kuzalisha takataka kwakiasi kibwa ukulinganisha na mikoa mingine nchini.

WANACHUO 27 "MIJO" KUANZA MITIHANI YAO JUMATATU

KUTOKA CHUMBA CHA HABARI

WANAFUNZI 27 wa Chuo Cha Uandishi wa Habri Mbeya(MIJO) wanatarajia kufanya mitihani ya kuhitimu Stashahada ya Juu katika Ujuzi wa Habari Jumatatu ya Novemba 8.

Akizungumza katika mahojiano maalum Mkurugenzi wa Chuo hicho Jonas
Mwasumbi alisema kozi hiyo imwetolewa kwa miezi 10 tangu mwezi Februari hadi Novemba mwaka huu.

Alisema kuwa mitihani hiyo ni maalumu kwa kukamilisha stashahada ya
juu ya Fani ya Uandishi wa Habari. Kozi hiyo imejikita katika masuala ya uandishi wa habari katika magazeti, redio na televisheni, maadili katika tasnia ya uandishi wa
habari, upigaji picha na mahusiani katika jamii (Public relations).

Aidha Mkurugenzi huyo alitoa wito kwa waandishi wa habari nchini
kujikita zaidi katika maadili ya fani hiyo ili kuepusha vurugu na
mafarakano katika jamii.

Imeandikwa na Godfrey Msomba
Kuhaririwa na Johnson Jabir.