Mbeya Institute Of Journalism (MIJO) inakukaribisha katika mwaka wa masomo wa Februari hadi Desemba 2010



Serikali ya Wanafunzi ya Chuo (SOMIJO) inakukaribisha kwa moyo mkunjufu katika tasnia hii ya Uandishi wa Habari zilizojawa na ukweli zenye kuleta maendeleo kwa mwananchi husika na taifa kwa ujumla.

Saturday, November 6, 2010

WANACHUO 27 "MIJO" KUANZA MITIHANI YAO JUMATATU

KUTOKA CHUMBA CHA HABARI

WANAFUNZI 27 wa Chuo Cha Uandishi wa Habri Mbeya(MIJO) wanatarajia kufanya mitihani ya kuhitimu Stashahada ya Juu katika Ujuzi wa Habari Jumatatu ya Novemba 8.

Akizungumza katika mahojiano maalum Mkurugenzi wa Chuo hicho Jonas
Mwasumbi alisema kozi hiyo imwetolewa kwa miezi 10 tangu mwezi Februari hadi Novemba mwaka huu.

Alisema kuwa mitihani hiyo ni maalumu kwa kukamilisha stashahada ya
juu ya Fani ya Uandishi wa Habari. Kozi hiyo imejikita katika masuala ya uandishi wa habari katika magazeti, redio na televisheni, maadili katika tasnia ya uandishi wa
habari, upigaji picha na mahusiani katika jamii (Public relations).

Aidha Mkurugenzi huyo alitoa wito kwa waandishi wa habari nchini
kujikita zaidi katika maadili ya fani hiyo ili kuepusha vurugu na
mafarakano katika jamii.

Imeandikwa na Godfrey Msomba
Kuhaririwa na Johnson Jabir.

No comments:

Post a Comment