Mbeya Institute Of Journalism (MIJO) inakukaribisha katika mwaka wa masomo wa Februari hadi Desemba 2010



Serikali ya Wanafunzi ya Chuo (SOMIJO) inakukaribisha kwa moyo mkunjufu katika tasnia hii ya Uandishi wa Habari zilizojawa na ukweli zenye kuleta maendeleo kwa mwananchi husika na taifa kwa ujumla.

Saturday, August 21, 2010

WAKAZI MBEYA WAMKUBALI SHITAMBALA

Na Abraham Mbugula

WANANCHI wa Jimbo la Mbeya Vijijini wamemtaja mgombea ubunge kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Sambwee Mwalyego Shitambala, kuwa ni tumaini jipya kwa maendeleo jimboni humo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wakazi wa kitongoji cha Mbalizi ambako kulifanyika uzinduzi wa kampeni za CHADEMA, walisema kuwa wanamtegemea Shitambala kuwa mwakilishi wao mzuri bungeni kutokana na sera zake alizozitoa na jinsi wanavyomfahamu.

Akizindua kampeni hizo zilizofanyika maeneo ya Tarafani Mbalizi Shitambala alisema kuwa anawataka watu wa Mbeya vijijini wawe wabunge wenyewe, ndipo wamtume yeye akawawakilishe bungeni.

Shitambala alisema kuwa katika kipindi chake cha uongozi atahakikisha anashughulikia kikamilifu suala la mbolea inayotolewa na serikali kwani watu wa Mbeya vijijini wanategemea zaidi kilimo.

Pia alisema kwamba atashughulikia suala la Elimu na kwamba atajitahidi kuwawezesha wanafunzi wanaoshindwa kufanya vizuri darasani kwa namna yoyote ile hata kama sio kuingia darasani ili mradi wasikae nyumbani na kuishia kushinda vijiweni.

Aidha Shitambala aliwataja wagombea udiwani kupitia chama hicho cha CHADEMA kuwa ni Difasi Mwakisale kwa kata ya Nsalala na Elia Mkono wa kata ya Utengule-Usongwe Mbeya vijijini.

No comments:

Post a Comment