Serikali ya Wanafunzi ya Chuo (SOMIJO) inakukaribisha kwa moyo mkunjufu katika tasnia hii ya Uandishi wa Habari zilizojawa na ukweli zenye kuleta maendeleo kwa mwananchi husika na taifa kwa ujumla.
Saturday, August 21, 2010
WAKAZI MBEYA WAMKUBALI SHITAMBALA
WANANCHI wa Jimbo la Mbeya Vijijini wamemtaja mgombea ubunge kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Sambwee Mwalyego Shitambala, kuwa ni tumaini jipya kwa maendeleo jimboni humo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wakazi wa kitongoji cha Mbalizi ambako kulifanyika uzinduzi wa kampeni za CHADEMA, walisema kuwa wanamtegemea Shitambala kuwa mwakilishi wao mzuri bungeni kutokana na sera zake alizozitoa na jinsi wanavyomfahamu.
Akizindua kampeni hizo zilizofanyika maeneo ya Tarafani Mbalizi Shitambala alisema kuwa anawataka watu wa Mbeya vijijini wawe wabunge wenyewe, ndipo wamtume yeye akawawakilishe bungeni.
Shitambala alisema kuwa katika kipindi chake cha uongozi atahakikisha anashughulikia kikamilifu suala la mbolea inayotolewa na serikali kwani watu wa Mbeya vijijini wanategemea zaidi kilimo.
Pia alisema kwamba atashughulikia suala la Elimu na kwamba atajitahidi kuwawezesha wanafunzi wanaoshindwa kufanya vizuri darasani kwa namna yoyote ile hata kama sio kuingia darasani ili mradi wasikae nyumbani na kuishia kushinda vijiweni.
Aidha Shitambala aliwataja wagombea udiwani kupitia chama hicho cha CHADEMA kuwa ni Difasi Mwakisale kwa kata ya Nsalala na Elia Mkono wa kata ya Utengule-Usongwe Mbeya vijijini.
Tuesday, August 17, 2010
WAWILI WAFA MBEYA
Na Johnson Jabir
WATU wawili wamefariki dunia juzi katika matukio mawili tofauti na wengine kujeruhiwa vibaya mkoani Mbeya.
Katika tukio la kwanza mkazi wa Ikuti-Iyunga Jijini Mbeya aliyefahamika kwa jina moja la Hassan anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 30 hadi 35, alifariki wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa Mbeya baada ya kupigwa na wananchi wenye hasira.
Mashuhuda wa tukio
Waliojeruhiwa katika tukio hilo, Amoni Damiani(31) mkazi wa Inyara-Iyunga na Nestory Mgaya(22) mkazi wa Nzovwe Jijini humo, ambao wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa huku wakiwa chini ya Ulinzi wa Polisi na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali hiyo.
Katika tukio jingine Mpanda baiskeli mkazi wa kijiji cha Lunwa, wilayani Mbarali aliyefahamika kwa jina la Fabian Mbikise(23) alikufa papo hapo baada ya kugongwa na gari lenye namba za usajili T 666 BCR, basi aina ya Yutong majira ya saa 1:30 usiku lililokuwa likiendeshwa na Mfaume Hamad katika barabara ya Mbeya-Iringa.
Kufuatia tukio
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi amethibitisha kutokea kwa matukio hayo na kuwataka wananchi kutojichukulia sheria mkononi na madereva kuwa waangalifu wawapo na barabarani ili kuleta usalama kwa walio ndani na nje ya vyombo vya usafiri.
Monday, August 16, 2010
VIJANA WAUNDANA UMOJA WAO
ZAIDI ya vijana 100 wa mikoa ya Mbeya, Dar es Salaam na Visiwani Zanzibar wameungana na kuunda Umoja utakaowasaidia kudai haki za vijana hapa nchini kutokana na vijana wengi kutotambua wajibu wao katika jamii.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti viongozi wa Kanda za Dar es Salaam na Mbeya, walisema umoja huo kwa sasa upo katika hatua za mwisho za usajili ambao utajikita zaidi katika masuala ya vijana walio na umri wa miaka 15 hadi 35.
Waliongeza kuwa umoja huo utajulikana kwa jina la MUHUVITA ambao utapigania vijana kujitambua, vilevile utajishughulisha na utunzaji wa Mazingira, utoaji wa elimu juu za dawa za kulevya kwani kundi kubwa linalotumia ni vijana ambao ni nguvu kazi ya Taifa la Tanzania.
“tangu tumepata uhuru hapa nchini mwaka 1961 hatujawahi kuona umoja wa vijana wenye madhumuni kama haya tulionayo ukianzishwa, na hata msajili mwenyewe ameshangaa na kusema hajawahi kuona vijana wakija na kusajili muungano wowote”.
Licha ya kujikita zaidi katika masuala ya vijana wenye umri wa kuanzia miaka 15 hadi 35 watajishughulisha pia na kupigania unyanyapaa wa watoto walio na umri chini ya miaka 15 hasa ukizingatia vitendo vya kikatili kwa watoto hao vimekuwa vikiongezeka siku baada ya siku, pia wakitoa elimu hiyo kwa wahusika kutasababisha watoto hao kukua vizuri huku wakitambua haki zao za msingi.
Hata hivyo wamejipanga kukabiliana na changamoto zitakazojitokeza na kusema madhumuni hasa ni kuirudisha nchi ya Tanzania katika hali yake kwani uzalendo umeonekana kupungua hususani kwa vijana ambao wengi wao wamekuwa wakitorokea ng’ambo kwa kudhani kuwa maisha bora yanapatikana huko na kuacha nafasi nzuri zilizopo bila kujali kwamba pato la taifa linapungua.
“vijana wengi wamekimbilia ng’ambo wakidhani watapata maendeleo lakini hakuna fursa nzuri kama zilizopo hapa Tanzania na wengine kwa kwenda huko wamepoteza maisha yao kitu ambacho ni hatari kwani kijana mmoja akipotea, nguvu kazi ya taifa inashuka kwa asilimia 90 ya uzalishaji”.
Kwa kuanza wameganyawa kanda tatu ambazo ni Dar es Salaam, Mbeya na Zanzibar huku wakitegemea kupanua zaidi matawi nchi nzima.
Saturday, August 14, 2010
85% YA VIZIWI HAJAANDIKISHWA KUPIGA KURA OKT. 31
ASILIMIA 85 ya watu wenye matatizo ya kusikia (viziwi) hawajaandikishwa kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani utakaofanyika Oktoba mwaka huu.
Akizungumza na Uhuru mwishoni mwa wiki hii Katibu wa Chama cha Viziwi mkoa wa Mbeya(CHAVITA) Today Wilson alisema viziwi wengi hawajaandikishwa katika daftari la kupigia kura kwa kuwa Serikali haijatoa kwa kundi hiloya elimu uraia.
Aliongeza kuwa CHAVITA mkoani Mbeya ina wanachama 3000 lakini walioandikishwa katika daftari ya kupigia kura ni 200.
Hata hivyo aliiomba Serikali na Tume ya Uchaguzi ya Taifa (NEC) kuliangalia kundi hilo ili haki ya msingi ya kupiga kura itumike ipasavyo kwa kuandaa maelekezo yatakayowasaidia kupiga kura mwaka huu.
Aidha alisema serikali inaweza kutumia hata mashirika mengine ya umma kusaidia kundi hilo.
85% DEAF PEOPLE AREN'T REGISTERED FOR TZ GENERAL ELECTION 2010
It is reported that members of Mbeya Society for the Deaf who are CCM members have not participated in the just ended opinion polls because of lack of civic education.
She also asked the respective organs to use her Society when giving civic education in order to reach the deaf.
MAGARI MATATU YAGONGANA, YAUA MMOJA NA KUJERUHI MBEYA

Walioshuhudia tukio hilo walisema gari lenye namba za usajili T823 AYZ na tera namba T814 AAS aina ya Leyland lilikuwa likiendeshwa na marehemu, liliigonga gari namba T128 ADY na tera namba T736 ALT aina Scania lililokuwa likiendeshwa na Issa Abdul (34) ambalo lilipoteza uelekeo na kuliigonga gari jingine lilikuwa mbele yake lenye namba za usajili T567 ATS na tera T451 ABF aina ya Scania Tanker lililokuwa likiendeshwa na Gustavu Mwalongo (42) na kupinduka.
Baada ya kupinduka marehemu alikufa papo hapo ambapo utingo wa gari lililosababisha ajali hilo aliyefahamika kwa jina la Saba Kasimu(30) alijeruhiwa na kulazwa katika hospitali ya Rufaa ya Mbeya na mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitalini hapo.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambayo ilisababishwa na gari hilo kushindwa kufunga breki katika mlima huo.
Wednesday, August 11, 2010
MFUNGO WA RAMADHANI WAANZA
Waislamu wanauanza mwezi wa tisa wa kalenda ya kiislamu ambao hujulikana zaidi kama mwezi wa Ramadhan kwa kujizuia kula na kunywa kuanzia alfajiri jua linapochomoza hadi jioni jua linapozama. Kufunga ni mojawapo ya nguzo tano za Uislamu.Kuanza na kumalizika kwa mwezi mtukufu wa Ramadhan hutegemea na kuandama kwa mwezi lakini kumekuwa na mgongano juu ya njia za kugundua kuandama kwa mwezi. Baadhi ya nchi hutaka mwezi lazima uonekane kwa macho na hukataa kutambua kuandama kwa mwezi kwa kutumia njia za kisayansi.
Nchini Saudi Arabia, televisheni ya taifa ya Al-Ekhbariyah ilitangaza kuwa baraza linalohusika na kuthibitisha kuandama kwa mwezi limetoa taarifa kuwa jumatano ndio mwanzo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.Nchi za Qatar, UAE, Bahrain, Kuwait, Misri, Syria, Lebanon, Yemen nazo zimetangaza kuwa mwezi wa Ramadhan unaanza leo jumatano.Baraza la Waislamu la Jordan lilitangaza kuwa mwezi haujaonekana nchini humo lakini kwakuwa umeonekana nchi za jirani basi na wao wataanza kufunga leo jumatano.Hata hivyo nchi ya Oman imetangaza kuwa wao wataanza kufunga alhamisi kwakuwa hawajauona mwezi nchi humo.
Licha ya mfungo huo ambao umeanza lakini nchini Pakistan wanauanza kwa machungu ya kupotelewa na ndugu na jamaa waliokufa katika mafuriko ambayo yamesababisha hasara kubwa na watu zaidi ya 1,600 walipoteza maisha.
SOMIJO inawatakia waislamu wote duniani mfungo mwema wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.
SH.900,000/- ZAMTOA ROHO
Mashuhuda wa tukio hilo walisema marehemu alikuwa Mfanyabiashara wa nyama ya bucha ambapo mauti yalimfika baada ya kuiba ng'ombe mmoja jike ambaye thamani yake ni shilingi 900,000/= mali ya mtu aliyefahamika kwa jina la Gwamaka Mwakaselela.
Walisema ng'ombe huyo aliibiwa kwa kuvunja zizi ambapo mara baada hapo alimchukua na kwenda naye maeneo ya Iwambi Jijini humo amabko ndiko walikomchinja na nyama yake waliipakia kwenye gari lenye namba za usajili T746 AAM aina ya Corola iliyokuwa ikiendeshwa na na mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Haule Kalamu(26).
Marehemu alifariki muda mfupi wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya.
Haule Kalamu ambaye ni dereva wa gari lililopakia nyama hiyo amekamatwa na gari lipo mikononi Jeshi la Polisi kwa hatua zaidi.
Kamanda la Polisi mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataka wasijichukulie sheria mkononi kwani ni kosa la kisheria.
Tuesday, August 10, 2010
MTOTO WA MIAKA 4 AKAMATWA AKIWANGA MBEYA

MAANDALIZI LIGI YA TAIFA YAANZA MBEYA

Akizungumza Mwenyekiti wa MUFA John Gondwe alisema Ligi ya Taifa ngazi ya wilaya inataka timu zijisajili kwanza kuthibitisha kushiriki mashindano hayo kwa kuanza kuchukua fomu ambazo gharama yake ni Shilingi 90,000.
Pia alizitaja timu ambazo tayari zimechukua fomu za usajili ni Eleven Boys SC, Mwanjelwa Stars, Airport Rangers, Uyole SC, Ilemi SC na Winners SC ambazo zimetoa zimethibitisha kushiriki.
“uchukaji wa fomu unaendelea vizuri ukilinganisha na mwaka jana kwani timu nyingi zimeonyesha moyo wa kushiriki kikamilifu, katika kiasi hicho cha fedha shilingi 20,000 ni kwa ajili ya kadi, shilingi 60,000 ni kwa ajili ya ada ya ushiriki na shilingi 10, 000 ya uanachama wa MUFA”.
Gondwe alitoa wito kwa timu ambazo bado zinasuasua kuthibitisha kushiriki zifanye haraka kwani mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu ni Agosti 23, mwaka huu.
Ligi ya Taifa ngazi ya wilaya itamalizika Septemba 31, mwaka huu.