Na Johnson Jabir
WATU wawili wamefariki dunia juzi katika matukio mawili tofauti na wengine kujeruhiwa vibaya mkoani Mbeya.
Katika tukio la kwanza mkazi wa Ikuti-Iyunga Jijini Mbeya aliyefahamika kwa jina moja la Hassan anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 30 hadi 35, alifariki wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa Mbeya baada ya kupigwa na wananchi wenye hasira.
Mashuhuda wa tukio
Waliojeruhiwa katika tukio hilo, Amoni Damiani(31) mkazi wa Inyara-Iyunga na Nestory Mgaya(22) mkazi wa Nzovwe Jijini humo, ambao wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa huku wakiwa chini ya Ulinzi wa Polisi na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali hiyo.
Katika tukio jingine Mpanda baiskeli mkazi wa kijiji cha Lunwa, wilayani Mbarali aliyefahamika kwa jina la Fabian Mbikise(23) alikufa papo hapo baada ya kugongwa na gari lenye namba za usajili T 666 BCR, basi aina ya Yutong majira ya saa 1:30 usiku lililokuwa likiendeshwa na Mfaume Hamad katika barabara ya Mbeya-Iringa.
Kufuatia tukio
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi amethibitisha kutokea kwa matukio hayo na kuwataka wananchi kutojichukulia sheria mkononi na madereva kuwa waangalifu wawapo na barabarani ili kuleta usalama kwa walio ndani na nje ya vyombo vya usafiri.
No comments:
Post a Comment