Mbeya Institute Of Journalism (MIJO) inakukaribisha katika mwaka wa masomo wa Februari hadi Desemba 2010



Serikali ya Wanafunzi ya Chuo (SOMIJO) inakukaribisha kwa moyo mkunjufu katika tasnia hii ya Uandishi wa Habari zilizojawa na ukweli zenye kuleta maendeleo kwa mwananchi husika na taifa kwa ujumla.

Saturday, November 13, 2010

SU KYI AACHIWA HURU


KUTOKA CHUMBA CHA HABARI

Kiongozi wa upinzani nchini Myanmar, Aung San Suu Kyi ameachiwa huru leo na uongozi wa kijeshi wa nchi hiyo.

Uongozi wa kijeshi nchini Myanmar umemuachia huru kiongozi wa upinzani nchini humo, Aung San Suu Kyi. Magari maalum leo yaliwasili katika nyumba ya kiongozi huyo iliyoko pembezoni mwa ziwa na polisi waliondoa vizuizi pamoja na senyenge.
Suu Kyi aliusalimia umati wa wafuasi wake wapatao 1,000 ambao walikuwa wamekusanyika katika lango la kuingilia kwenye nyumba hiyo. Mshindi huyo wa Tuzo ya Amani ya Nobel, ametumikia kifungo cha nyumbani kwa takriban miaka 21.
Kitendo cha kuachiwa kwa mtetezi huyo wa demokrasia kimepongezwa na viongozi mbalimbali wa Ulaya, Marekani na Jumuiya ya mataifa ya Kusini-Mashariki mwa Asia-ASEAN.
Kifungo hicho cha nyumbani dhidi ya Suu Kyi kimemalizika ikiwa ni wiki moja baada ya vyama vinavyoungwa mkono na uongozi wa kijeshi wa Myanmar kushinda katika uchaguzi ambao mataifa ya Magharibi yameuelezea kama wa uzandiki.

Imeandikwa na: Grace Kabogo (AFP, DPA)

MBOWE KIONGOZI KAMBI YA UPINZANI BUNGENI

KUTOKA CHUMBA CHA HABARI
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimemteua mbunge wa Hai, Freman Mbowe kuwa kiongozi wa kambi ya upinzani katika bunge la 10 la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mbali na kuteuliwa kwa mbunge huyo pia chama hicho kimemteua mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto kuwa makamu wa kambi hiyo bungeni.Hata hivyo uteuzi huo umefanya kambi ya upinzani bungeni kumeguka kwa vyama vingine kutokubaliana na uteuzi huo, na kudaiwa kuundwa kambi mbili za upinzani.Awali Mbunge wa Wawi (CUF), Hamad Rashid Mohamed, ndiye alikuwa kiongozi mkuu wa usemaji kambi ya upinzani na Aliyekuwa mbunge wa Karatu, Wilbrod Slaa alikuwa naibu wake.


Imeandikwa na :Johnson Jabir

Saturday, November 6, 2010

Agatha Mboya

ZAIDI ya Sh 50 billioni zitatumika katika kukamilisha mradi mkubwawa maji unaojengwa katika Jiji la Mbeya.

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka (Uwasa) katika Jiji laMbeya, Simion Shauri alisema mradi huo ulioanza kujengwa Septemba2008 unatarajia kukamilika mwakani na kwamba utawezesha wakazi wote wajiji hilo kupata maji safi na salama katika kipindi chote cha mwaka.

Shauri alisema fedha za ujenzi wa mradi huo wa maji zimetolewa naShirika la Kijerumani KFW pamoja na Umoja wa Nchi za Ulaya (EU) kwakushirikiana na Benki ya Dunia.Kwa mujibu wa maelezo ya Shauri kukamilika kwa mradi huo wa majikutaongeza kiasi cha maji kutoka wastani wa mita 32,000 kwa siku zasasa hadi kufikia mita za ujazo 49,000 kwa siku.

Aliongeza kusema kuwa chini ya mradi huo mkandarasi kutoka nchini UfaransaSogea Satom anajenga mitambo ya kisasa yenye uwezo mkubwa wa kusukumamaji katika vyanzo vya Nkwanana Mwatezi, na LunjiMkandarasi huyo pia anajenga mitambo ya kisasa ya kutibia maji katikavyanzo vya Meta Sisimba, Sai, Lunji, Mwatezi, Iduda na Nsalagapamoja na kujenga vituo vipya vya kusukuma maji katika eneo la SwayaNelotia, Nsalaga na ImetaAlisema matanki saba makubwa ya kuhifadhia maji yanajengwa katikamaeneo ya Veta, Forest mpya, Iwambi, Imeta, Iganjo, Nsoho, na Iduda.

“Mradi huo pia unaongeza mtandao wa maji kwa kuunganisha na mabombayenye urefu wa kilomita zaidi ya 37 na kujenga viungo kwa wateja wapyana kupanua mabwawa ya kutibu maji taka katika eneo la Kalobe ilikuepusha magonjwa ya milipuko kwa wakazi wanaoishi katika maeneohayo,”alisema.

Alisema fedha hizo pia zitatumika katika kununua vitendea kazi kwaajili ya matengezo ya mtandao wa mabomba na shughuli za umeme namagari matatu ya maji taka pamoja na ujenzi wa vyoo mashuleni naujenzi wa vyumba vya kuishi watumishi na ujenzi karakana za kupimausahihi wa dira za maji.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo wa Mamlaka ya Maji safi na Majitakajijini Mbeya, utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 80 na zaidiya jumla ya Sh 27 bilioni zimekwishalipwa na gharama za kutekelezamradi mzima ni zaidi ya Sh 56 milioni. Awamu ya pili ya ujenziitagharimu Sh 13 bilioni.

JIJI LA MBEYA LAKABILIWA NA UKATA WA MAGARI YA TAKA

Na Onesmo Alfred.

LICHA ya mkoa wa mbeya kuwa jiji lakini bado unakabiliwa na uhaba mkubwa wa magari ya kubeabea takataka jijini hapa .

Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana baadhi ya wakazi wa maaeneo ya Mwanjelwa na Soweto wamesema hali hiyo imekuwa ikiwafanya wao kuwapa kikwazo kutokana na hali ya baadhi ya maghuba kujaa taakataka na nyigine kumwangwa nje.

“Mimi hali hii inanikera sana kwasababu husababisha biashara yangu kwenda vibaya kutokana na wateja wangu kukimbia kutokana na ghuba hili kujaa taka na kutoa harufu kali pia kutokana na biashara yangu ya mamalishe nina somesha watoto watatu wakiwemo wa sekondari wawili na wa shule ya msingi mmoja hivyo kukosa wateja kwangu hunisababishia kukosa ada ya watoto wangu, ”alisema.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jiji la mbeya Juma Idd alisema halmashauri ilikuwa ikikabiliwa na uhaba mkubwa wa magari yakubebea takataka.

Idd alisema hivi sasa halmashauri iko kwenye mikakati yakununua magari ilikuweza kukabiliana na hali hiyo ilikuweza kuufanya mkoa wa mbeya kuwa nahadhi ya jiji na kuwa halmashauri ina mpango wa wakuwa na gari kumi na sita haya niya side roder(yakubebae takataka) na skip master

Alisema halmashauri ilikuwa na magari matatu yakubebea takataka (side roder) likiwepo moja kwaajili ya kubebea maghuba (skip master) ilikuweza kukabiliana na hali hiyo ya kero ya takataka hizo.

Ambapo amesema jiji lina uwezo wakuzalisha tani 1260 kwa siku hivyo gari moja lina uwezo wakubebe safari tatu ambazo ni sawa na tani 14 kwa siku halmashauri ina uwezo wakubeba tani 420 kwa siku

Mkurugenzi alizitaja baadhi ya sababu ambazo husababisha uzalishaji huo wataka kuwa ni idadi kubwa ya watu katika jiji la mbeya likemo lilela kushamili kwa biashara katika jiji la mbeya.

Aidha alisema kuwa jiji la mbeya linashika nafasi ya tatu kwabiashara kitaifa hivyonilahisi sana kuzalisha takataka kwakiasi kibwa ukulinganisha na mikoa mingine nchini.

WANACHUO 27 "MIJO" KUANZA MITIHANI YAO JUMATATU

KUTOKA CHUMBA CHA HABARI

WANAFUNZI 27 wa Chuo Cha Uandishi wa Habri Mbeya(MIJO) wanatarajia kufanya mitihani ya kuhitimu Stashahada ya Juu katika Ujuzi wa Habari Jumatatu ya Novemba 8.

Akizungumza katika mahojiano maalum Mkurugenzi wa Chuo hicho Jonas
Mwasumbi alisema kozi hiyo imwetolewa kwa miezi 10 tangu mwezi Februari hadi Novemba mwaka huu.

Alisema kuwa mitihani hiyo ni maalumu kwa kukamilisha stashahada ya
juu ya Fani ya Uandishi wa Habari. Kozi hiyo imejikita katika masuala ya uandishi wa habari katika magazeti, redio na televisheni, maadili katika tasnia ya uandishi wa
habari, upigaji picha na mahusiani katika jamii (Public relations).

Aidha Mkurugenzi huyo alitoa wito kwa waandishi wa habari nchini
kujikita zaidi katika maadili ya fani hiyo ili kuepusha vurugu na
mafarakano katika jamii.

Imeandikwa na Godfrey Msomba
Kuhaririwa na Johnson Jabir.

Saturday, August 21, 2010

WAKAZI MBEYA WAMKUBALI SHITAMBALA

Na Abraham Mbugula

WANANCHI wa Jimbo la Mbeya Vijijini wamemtaja mgombea ubunge kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Sambwee Mwalyego Shitambala, kuwa ni tumaini jipya kwa maendeleo jimboni humo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wakazi wa kitongoji cha Mbalizi ambako kulifanyika uzinduzi wa kampeni za CHADEMA, walisema kuwa wanamtegemea Shitambala kuwa mwakilishi wao mzuri bungeni kutokana na sera zake alizozitoa na jinsi wanavyomfahamu.

Akizindua kampeni hizo zilizofanyika maeneo ya Tarafani Mbalizi Shitambala alisema kuwa anawataka watu wa Mbeya vijijini wawe wabunge wenyewe, ndipo wamtume yeye akawawakilishe bungeni.

Shitambala alisema kuwa katika kipindi chake cha uongozi atahakikisha anashughulikia kikamilifu suala la mbolea inayotolewa na serikali kwani watu wa Mbeya vijijini wanategemea zaidi kilimo.

Pia alisema kwamba atashughulikia suala la Elimu na kwamba atajitahidi kuwawezesha wanafunzi wanaoshindwa kufanya vizuri darasani kwa namna yoyote ile hata kama sio kuingia darasani ili mradi wasikae nyumbani na kuishia kushinda vijiweni.

Aidha Shitambala aliwataja wagombea udiwani kupitia chama hicho cha CHADEMA kuwa ni Difasi Mwakisale kwa kata ya Nsalala na Elia Mkono wa kata ya Utengule-Usongwe Mbeya vijijini.

Tuesday, August 17, 2010

WAWILI WAFA MBEYA

Na Johnson Jabir

WATU wawili wamefariki dunia juzi katika matukio mawili tofauti na wengine kujeruhiwa vibaya mkoani Mbeya.


Katika tukio la kwanza mkazi wa Ikuti-Iyunga Jijini Mbeya aliyefahamika kwa jina moja la Hassan anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 30 hadi 35, alifariki wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa Mbeya baada ya kupigwa na wananchi wenye hasira.

Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa marehemu akiwa na wenzake wawili walivunja na kuiba masanduku ya chupa za bia tupu katika kiwanda cha kutengeneza bia (TBL) majira ya saa 5:00 usiku, ambapo thamani ya masunduku haikujulikana mara moja.

Waliojeruhiwa katika tukio hilo, Amoni Damiani(31) mkazi wa Inyara-Iyunga na Nestory Mgaya(22) mkazi wa Nzovwe Jijini humo, ambao wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa huku wakiwa chini ya Ulinzi wa Polisi na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali hiyo.

Katika tukio jingine Mpanda baiskeli mkazi wa kijiji cha Lunwa, wilayani Mbarali aliyefahamika kwa jina la Fabian Mbikise(23) alikufa papo hapo baada ya kugongwa na gari lenye namba za usajili T 666 BCR, basi aina ya Yutong majira ya saa 1:30 usiku lililokuwa likiendeshwa na Mfaume Hamad katika barabara ya Mbeya-Iringa.

Kufuatia tukio hilo dereva wa basi hilo alikimbia na kulitelekeza basi hilo ambalo hata hivyo liliendeshwa na dereva wa pili ambaye hakufahamika mara moja na kufikishwa katika kituo cha polisi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi amethibitisha kutokea kwa matukio hayo na kuwataka wananchi kutojichukulia sheria mkononi na madereva kuwa waangalifu wawapo na barabarani ili kuleta usalama kwa walio ndani na nje ya vyombo vya usafiri.

Monday, August 16, 2010

VIJANA WAUNDANA UMOJA WAO

Na Johnson Jabir

ZAIDI ya vijana 100 wa mikoa ya Mbeya, Dar es Salaam na Visiwani Zanzibar wameungana na kuunda Umoja utakaowasaidia kudai haki za vijana hapa nchini kutokana na vijana wengi kutotambua wajibu wao katika jamii.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti viongozi wa Kanda za Dar es Salaam na Mbeya, walisema umoja huo kwa sasa upo katika hatua za mwisho za usajili ambao utajikita zaidi katika masuala ya vijana walio na umri wa miaka 15 hadi 35.

Waliongeza kuwa umoja huo utajulikana kwa jina la MUHUVITA ambao utapigania vijana kujitambua, vilevile utajishughulisha na utunzaji wa Mazingira, utoaji wa elimu juu za dawa za kulevya kwani kundi kubwa linalotumia ni vijana ambao ni nguvu kazi ya Taifa la Tanzania.

“tangu tumepata uhuru hapa nchini mwaka 1961 hatujawahi kuona umoja wa vijana wenye madhumuni kama haya tulionayo ukianzishwa, na hata msajili mwenyewe ameshangaa na kusema hajawahi kuona vijana wakija na kusajili muungano wowote”.

Licha ya kujikita zaidi katika masuala ya vijana wenye umri wa kuanzia miaka 15 hadi 35 watajishughulisha pia na kupigania unyanyapaa wa watoto walio na umri chini ya miaka 15 hasa ukizingatia vitendo vya kikatili kwa watoto hao vimekuwa vikiongezeka siku baada ya siku, pia wakitoa elimu hiyo kwa wahusika kutasababisha watoto hao kukua vizuri huku wakitambua haki zao za msingi.

Hata hivyo wamejipanga kukabiliana na changamoto zitakazojitokeza na kusema madhumuni hasa ni kuirudisha nchi ya Tanzania katika hali yake kwani uzalendo umeonekana kupungua hususani kwa vijana ambao wengi wao wamekuwa wakitorokea ng’ambo kwa kudhani kuwa maisha bora yanapatikana huko na kuacha nafasi nzuri zilizopo bila kujali kwamba pato la taifa linapungua.

“vijana wengi wamekimbilia ng’ambo wakidhani watapata maendeleo lakini hakuna fursa nzuri kama zilizopo hapa Tanzania na wengine kwa kwenda huko wamepoteza maisha yao kitu ambacho ni hatari kwani kijana mmoja akipotea, nguvu kazi ya taifa inashuka kwa asilimia 90 ya uzalishaji”.

Kwa kuanza wameganyawa kanda tatu ambazo ni Dar es Salaam, Mbeya na Zanzibar huku wakitegemea kupanua zaidi matawi nchi nzima.

Saturday, August 14, 2010

85% YA VIZIWI HAJAANDIKISHWA KUPIGA KURA OKT. 31

Na Wazo Mboya

ASILIMIA 85 ya watu wenye matatizo ya kusikia (viziwi) hawajaandikishwa kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani utakaofanyika Oktoba mwaka huu.

Akizungumza na Uhuru mwishoni mwa wiki hii Katibu wa Chama cha Viziwi mkoa wa Mbeya(CHAVITA) Today Wilson alisema viziwi wengi hawajaandikishwa katika daftari la kupigia kura kwa kuwa Serikali haijatoa kwa kundi hiloya elimu uraia.

Aliongeza kuwa CHAVITA mkoani Mbeya ina wanachama 3000 lakini walioandikishwa katika daftari ya kupigia kura ni 200.

Hata hivyo aliiomba Serikali na Tume ya Uchaguzi ya Taifa (NEC) kuliangalia kundi hilo ili haki ya msingi ya kupiga kura itumike ipasavyo kwa kuandaa maelekezo yatakayowasaidia kupiga kura mwaka huu.

Aidha alisema serikali inaweza kutumia hata mashirika mengine ya umma kusaidia kundi hilo.

85% DEAF PEOPLE AREN'T REGISTERED FOR TZ GENERAL ELECTION 2010




By Joseph Elijah Kitha

More than 85 percent of the deaf are believed to have not registered in the Tanzania permanent register of voters.

The Mbeya Regional Secretary of the Society for the Deaf [CHAVITA], Today Wilson claimed here recently that most of the deaf have not registered because the government has not provided them with enough civic education.

According to Today, the society in Mbeya has 3,000 members who are acceptable by the constitution of Tanzania to vote but only 200 members have registered.
It is reported that members of Mbeya Society for the Deaf who are CCM members have not participated in the just ended opinion polls because of lack of civic education.

Today has asked the Government and National Electoral Commission to involve specialized instructors for the deaf in civic education provision.
She also asked the respective organs to use her Society when giving civic education in order to reach the deaf.

“Government can also use the Foundation for the Civil Society [FCS] to provide civic education, in order to reach the targeted people’’, said Today.

MAGARI MATATU YAGONGANA, YAUA MMOJA NA KUJERUHI MBEYA


MKAZI aliyefahamika kwa jina moja la Ramadhani ambaye umri wake hakupatikana mara moja amekufa papo hapo na mmoja kujeruhiwa mwishoni mwa juma majira ya saa 6:15 mchana baada ya gari alilokuwa akiendesha kupinduka katika eneo la Mlima Nyoka, Mbeya Vijijini barabara ya Mbeya-Iringa.


Walioshuhudia tukio hilo walisema gari lenye namba za usajili T823 AYZ na tera namba T814 AAS aina ya Leyland lilikuwa likiendeshwa na marehemu, liliigonga gari namba T128 ADY na tera namba T736 ALT aina Scania lililokuwa likiendeshwa na Issa Abdul (34) ambalo lilipoteza uelekeo na kuliigonga gari jingine lilikuwa mbele yake lenye namba za usajili T567 ATS na tera T451 ABF aina ya Scania Tanker lililokuwa likiendeshwa na Gustavu Mwalongo (42) na kupinduka.


Baada ya kupinduka marehemu alikufa papo hapo ambapo utingo wa gari lililosababisha ajali hilo aliyefahamika kwa jina la Saba Kasimu(30) alijeruhiwa na kulazwa katika hospitali ya Rufaa ya Mbeya na mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitalini hapo.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambayo ilisababishwa na gari hilo kushindwa kufunga breki katika mlima huo.

Wednesday, August 11, 2010

MFUNGO WA RAMADHANI WAANZA

Waislamu duniani jana walianza mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan huku wengine wakitarajiwa kuanza kufunga leo alhamisi.

Waislamu wanauanza mwezi wa tisa wa kalenda ya kiislamu ambao hujulikana zaidi kama mwezi wa Ramadhan kwa kujizuia kula na kunywa kuanzia alfajiri jua linapochomoza hadi jioni jua linapozama. Kufunga ni mojawapo ya nguzo tano za Uislamu.Kuanza na kumalizika kwa mwezi mtukufu wa Ramadhan hutegemea na kuandama kwa mwezi lakini kumekuwa na mgongano juu ya njia za kugundua kuandama kwa mwezi. Baadhi ya nchi hutaka mwezi lazima uonekane kwa macho na hukataa kutambua kuandama kwa mwezi kwa kutumia njia za kisayansi.

Nchini Saudi Arabia, televisheni ya taifa ya Al-Ekhbariyah ilitangaza kuwa baraza linalohusika na kuthibitisha kuandama kwa mwezi limetoa taarifa kuwa jumatano ndio mwanzo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.Nchi za Qatar, UAE, Bahrain, Kuwait, Misri, Syria, Lebanon, Yemen nazo zimetangaza kuwa mwezi wa Ramadhan unaanza leo jumatano.Baraza la Waislamu la Jordan lilitangaza kuwa mwezi haujaonekana nchini humo lakini kwakuwa umeonekana nchi za jirani basi na wao wataanza kufunga leo jumatano.Hata hivyo nchi ya Oman imetangaza kuwa wao wataanza kufunga alhamisi kwakuwa hawajauona mwezi nchi humo.

Licha ya mfungo huo ambao umeanza lakini nchini Pakistan wanauanza kwa machungu ya kupotelewa na ndugu na jamaa waliokufa katika mafuriko ambayo yamesababisha hasara kubwa na watu zaidi ya 1,600 walipoteza maisha.

SOMIJO inawatakia waislamu wote duniani mfungo mwema wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.

SH.900,000/- ZAMTOA ROHO

MKAZI wa Kabwe Jijini Mbeya aliyefahamika kwa jina la Ramadhani Mwakyusa (25) amefariki dunia kwa kupigwa na wananchi wenye hasira juzi majira ya saa 12:45 jioni.
Mashuhuda wa tukio hilo walisema marehemu alikuwa Mfanyabiashara wa nyama ya bucha ambapo mauti yalimfika baada ya kuiba ng'ombe mmoja jike ambaye thamani yake ni shilingi 900,000/= mali ya mtu aliyefahamika kwa jina la Gwamaka Mwakaselela.

Walisema ng'ombe huyo aliibiwa kwa kuvunja zizi ambapo mara baada hapo alimchukua na kwenda naye maeneo ya Iwambi Jijini humo amabko ndiko walikomchinja na nyama yake waliipakia kwenye gari lenye namba za usajili T746 AAM aina ya Corola iliyokuwa ikiendeshwa na na mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Haule Kalamu(26).

Marehemu alifariki muda mfupi wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya.

Haule Kalamu ambaye ni dereva wa gari lililopakia nyama hiyo amekamatwa na gari lipo mikononi Jeshi la Polisi kwa hatua zaidi.

Kamanda la Polisi mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataka wasijichukulie sheria mkononi kwani ni kosa la kisheria.

Tuesday, August 10, 2010

MTOTO WA MIAKA 4 AKAMATWA AKIWANGA MBEYA

Mtoto aliyefahamika kwa jina la Midian Obadia(4) amekutwa akiwanga jana majira ya saa 5:00 usiku katika kata ya Igawilo Jijini Mbeya ndani ya nyumba ya mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Mama Sanga.


Mtoto huyo amekutwa akiwa amevaa mfuko wa saruji uliotobolewa juu huku kichwa chake kikionekana kimepakwa vitu vyeupe kama unga, alikusanya watu wa mitaa iliyo karibu .


Pia vitu mbalimbali ambavyo ni sindano,matunguli,mavi ya punda, vitu kama mafuta na barua ambazo zinahusu vikao vya kichawi vitakavyofanyika Jumamosi kwa ajili ya kutathmini vifo vya watu waliowauwa kwa njia ya kuwatoa mimba


Imebainika kuwa Mkazi wa Mtaa wa Mwanyanje kata ya Iganjo iliyopo Uyole jijini Mbeya aliyefahamika kwa jina Bupe Njoka (54) anadaiwa kumpandikiza uchawi mjukuu wake huyo wa kiume.Bibi huyo anayedaiwa kumpandikiza mtoto huyo uchawi amekana kuhusika na vitendo hivyo ambapo alilazimika kuishi na mtoto huyo baada ya wazazi wake kutengana.


Mwenyekiti wa mtaa huo Antony Mwalyambi alimtaka mtoto huyo aende

MAANDALIZI LIGI YA TAIFA YAANZA MBEYA


CHAMA cha soka wilaya ya Mbeya Mjini (MUFA) kimeanza maandalizi ya Ligi ya Taifa Ngazi ya Wilaya kwa kusajili timu zitazojiandaa na ligi hiyo ambayo itaanza kutimua vumbi Agosti 28 katika uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.


Akizungumza Mwenyekiti wa MUFA John Gondwe alisema Ligi ya Taifa ngazi ya wilaya inataka timu zijisajili kwanza kuthibitisha kushiriki mashindano hayo kwa kuanza kuchukua fomu ambazo gharama yake ni Shilingi 90,000.


Pia alizitaja timu ambazo tayari zimechukua fomu za usajili ni Eleven Boys SC, Mwanjelwa Stars, Airport Rangers, Uyole SC, Ilemi SC na Winners SC ambazo zimetoa zimethibitisha kushiriki.


“uchukaji wa fomu unaendelea vizuri ukilinganisha na mwaka jana kwani timu nyingi zimeonyesha moyo wa kushiriki kikamilifu, katika kiasi hicho cha fedha shilingi 20,000 ni kwa ajili ya kadi, shilingi 60,000 ni kwa ajili ya ada ya ushiriki na shilingi 10, 000 ya uanachama wa MUFA”.


Gondwe alitoa wito kwa timu ambazo bado zinasuasua kuthibitisha kushiriki zifanye haraka kwani mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu ni Agosti 23, mwaka huu.
Ligi ya Taifa ngazi ya wilaya itamalizika Septemba 31, mwaka huu.

Saturday, May 29, 2010

AMNESTY INTERNATIONAL LATOA RIPOTI YA 2009

Na DW- UJERUMANI

Shirika la Amnesty International limeupongeza mwaka jana 2009 kama mwaka muhimu kuhusu haki kwenye ripoti yake iliyotolewa jana. Shirika hilo limesema maafisa wa usalama barani Afrika waliua bila hofu ya kuadhibiwa

Kwenye ripoti ya mwaka 2010 kuhusu hali ya haki za binadamu ulimwenguni shirika la kutetea haki za binadamu, Amnesty International, lenye makao yake makuu mjini London Uingereza, limeueleza waranti wa mahakama ya ICC wa mwaka 2009 wa kukamatwa rais wa Sudan Omar al Bashir kujibu mashtaka ya uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu, kuwa tukio kubwa muhimu linalodhihirisha kwamba hata marais walio madarakani wako chini ya sheria.

Mkuu wa shirika la Amnesty International tawi la Ujerumani, Monika Lüke anasema, "Ufanisi mkubwa ni waranti wa kimataifa wa kukamatwa rais wa Sudan Omar al Bashir mwezi Machi mwaka jana uliotoa ishara kwa wote wanaowatesa na kuwatia gerezani wengine kwamba hawawezi kufanya hivyo bila kuadhibiwa. Ni mara ya kwanza kwa rais aliye madarakani kukabiliwa na waranti ya mahakama ya kimataifa."

Shirika hilo limezitaka serikali mbalimbali kusaini mkataba unaoitambua kikamilifu mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita mjini The Hague Uholanzi ili kuhakikisha uhalifu chini ya sheria ya kimataifa unaweza kushughulikiwa mahala popote duniani. Marekani, Urusi, China, Indonesia na Uturuki ni miongoni mwa mataifa ambayo hayajasaini mkataba huo.

Bi Monika Lüke ameikosoa Urusi, Sri Lanka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa ukiukaji wa haki za binadamu. Ameongeza kwamba hali ya haki za binadamu imeendelea kuwa mbaya nchini Urusi chini ya utawala wa rais Dmitry Medvedev.
Vikosi vya usalama na maafisa wa polisi barani Afrika wamelaumiwa kwa kuwaua mamia ya watu mwaka jana 2009 lakini hawakuchunguzwa kutokana na utamaduni wa kutojali kuadhibiwa wala kuchukuliwa hatua yoyote.

Ripoti imegusia mauaji ya kiholela yaliyofanywa kwenye uwanja wa michezo katika mji mkuu wa Guinea, Conakry mwezi Septemba mwaka jana ambapo zaidi ya watu 150 waliokuwa wakishiriki kwenye maandamano waliuwawa na wanawake wakabakwa hadharani. Shirika la Amnesty International linasema uhalifu dhidi ya binadamu ulifanyika na kupendekeza kesi hiyo iwasilishwe kwa mahakama ya ICC mjini The Hague.

Shirika hilo limeelezea wasiwasi wake kuhusu hali nchini Nigeria, likisema mamia ya watu huuwawa kila mwaka mikononi mwa polisi. Cameroon pia imenyoshewa kidole cha lawama huku kukiwa hakuna dalili yoyote ya serikali kuanza kuchunguza mauaji ya watu takriban 100 mnamo mwaka 2008 wakati wa operesheni dhidi ya waandamanaji.

Nchini Kenya, shirika la Amnesty International linasema serikali imeshindwa kuchunguza kikamilifu ukiukaji wa haki za binadamu wakati wa machafuko ya baada ya uchaguzi wa mwaka 2007 na 2008 ambapo zaidi ya watu 1,000 waliuwawa.

Ripoti pia imeitaja Madagascar ikisema hakuna uchunguzi huru ulioanzishwa kuchunguza mauaji ya watu wasiopungua 31, mnamo Februari 7 mwaka jana wakati wanajeshi wa nchi hiyo walipowafyatulia risasi waandamanaji walipokuwa wakiandamana katika ikulu ya rais mjini Antananarivo.

Huko Zimbabwe hali ya haki za binadamu iliboreka kidogo kufuatia kuundwa serikali ya umoja wa kitaifa mwezi Februari mwaka jana. Hata hivyo kuteswa na kutishwa kwa watetezi wa haki za binadamu, wanaharakati wa kisiasa na wafuasi wa chama cha upinzani, Movement for Democratic Change, MDC, cha waziri mkuu Morgan Tsvangirani, kuliendelea.

Rais wa Marekani Barack Obama amekosolewa kwa kushindwa kuifunga jela ya Guantanamo Bay nchini Cuba. Wafungwa 198 waliendelea kuzuiliwa katika gereza hilo kufikia mwisho wa mwaka jana licha ya ahadi ya utawala wa Obama kulifunga kufikia Januari 22 mwaka huu.
Iran imekosolewa kwa kuwakandamiza, kuwatesa, kuwakamata na kuwaua waandanaji baada ya uchaguzi wa rais wa mwezi Juni mwaka jana. Maafisa wamekosolewa kwa kubana uhuru wa kujieleza, kuzuia mawasiliano ya simu za mkono na mtandao wa intaneti.

Barani Asia China iliongeza shinikizo dhidi ya wapinzani wa serikali kwa kuwazuilia na kuwatesa wanaharakati wa haki za binadamu. Maelfu ya watu wamekimbia mateso na hali ngumu ya kiuchumi nchini Korea Kaskazini na Myanmar.Katika mzozo wa Gaza na kusini mwa Israel, vikosi vya Israel na makundi ya wapiganaji wa Palestina waliua kinyume cha sheria na kuwajeruhi raia. Maelfu ya raia wanakabiliwa na mateso na ukiukaji wa haki kutokana na ongezeko la machafuko ya kundi la Taliban nchini Afghanistan na Pakistan

MZEE PWAGU KATUTOKA


Na Johnson Jabir
MIJO, TANZANIA

Aliyekuwa mwigizaji mahiri redioni Rajab Kibwana Hatia al maaruf Mzee Pwagu amefariki dunia.Mzee Pwagu amefariki Ijumaa, Mei 28, 2010 katika hospitali ya Amana jijini Dar Es Salaam kutokana na kusumbuliwa na kwikwi na hali ya uzee.

Mzee Pwagu alikuwa anakamilisha pacha wake Mzee Pwaguzi katika kipindi cha redio kilichokuwa maafuru sana miaka ya sitini hadi themanini kilichojulikana kwa jina la Pwagu na Pwaguzi.

Kipindi hicho kilikuwa kikirushwa hewani kila siku ya Jumamosi saa kumi na moja na dakika arobaini na tano jioni hadi saa kumi na mbili kamili (11:45 - 12:00) kupitia Redio Tanzania Dar Es Salaam (RTD). Kwa mara ya kwanza kipindi hicho kilianza kusikika mwaka 1966 na kilipendwa kusikilizwa na watu wa rika zote kutokana na kuelimisha na kutoa burudani inayogusa maisha ya kila siku ya Mtanzania, hadi mwaka 1980 kilipokoma.

Marehemu alikuwa akiishi Kigogo Mbuyuni jijini Dar Es Salaam na anatarajiwa kuzikwa kesho.Apumzike pema Rajab Kibwana Hatia/Mzee Pwagu.

Tuesday, April 13, 2010

MHINDI WA KAPUNGA ASEMA AWEZA KUUA YEYOTE AKIMKOROFISHA

Na Johnson Jabir/Mike mbughi
MBEYA, TANZANIA

WANANCHI wanaolizunguka shamba la Kapunga Wilayani Mbarali, mkoani Mbeya wamemlalamikia msimamizi wa Shirika hilo Badri Dart kwa unyanyasaji na kusababisha uhasama baina ya wananchi na shirika hilo.

Uchunguzi uliofanywa na JAIZMELA umebaini kuwa kiongozi huyo mwenye asili ya ki-Asia amekuwa mwiba kwa wafanyakazi wa kipato cha chini kwa unyanyasaji na kuwatuhumu kuwa wafanyakazi hao ni wezi.

Baadhi ya wananchi waliofanya mahojiano na JAIZMELA kwa sharti la kutotaja majina yao walisema kuwa tokea Badri ajiunge na kampuni hiyo mwaka 2007 akijitambulisha kuwa yeye ni Afisa mipaka wa shirika hilo amekuwa akizua mitafaruku mbali mbali ikiwemo ya wakazi wa Mapogoro hasa jamii ya wasukuma ambao walidai walipokonywa mashamba yao na mhindi huyo.

Wananchi hao walidai kuwa kiongozi huyo amekuwa akiwatishia kuua mtu kama wataendelea kupita kwenye mashamba ya shirika hilo wakati ndiyo njia pekee ya kupita kwenda kwenye mashamba yao.

Waliongeza kuwa Badri amekuwa akiwatuhumu na kuwakashfu wananchi hao kuwa ni wezi na kudai kuwa yeye hawezi kutishiwa na mtu yeyote kwa kuwa yuko pamoja na viongozi wa nchi ikiwa ni pamoja na mtu mmoja aliyetajwa kwa jina la Maheshi Patel.

“Huyu kijana amekuwa akitukashfu sana kwa kusema sisi wakazi wa Kapunga ni wezi, inasikitisha sana maana tupo hapa kapunga mda mlefu hatujawahi kuambiwa na mtu yeyote maneno kama hayo” alisema mzee mmoja jina linahifadhiwa.

“Kwanza amelifanya shirika lichukiwe na wanchi wa eneo hili kwa sababu ya kashifa zake na kauli ya kusema yuko pamoja na viongozi wetu kitu labda kwa kuwa baadhi ya viongozi wanalima kwenye mashamba hayo na akajenga urafiki na viongozi hao ndiyo maana anakiburi” aliongeza mzee mwingine jina linahifadhiwa.

Kapunga bila Badri Dart inawezekana tena kutakuwa na amani nje na hata ndani ya shirika maana hata wafanyakazi wanaendeshwa kama watumwa kwa kweli haiwezekani mtu mmoja akaivuruga kampuni kwa mitafaruku na wananchi, kwanini viongozi wengine wasishutumiwe? Alisema kijana wa Kimasai.

JAIZMELA ilifanya mahojiano na wafanyakazi wa shirika hilo kwa sharti la kutotaja majina yao na kueleza kuwa kiongozi huyo amekuwa akiwanyanyasa vilivyo na kuwashutumu mara kwa mara kuwa ni wezi huku wengine wakifikishwa mahakamani.

Wafanyakazi hao walisema kuwa amekuwa akiwafanyisha kazi kama watumwa akidai asiyetaka aache kazi zake milango iko iko wazi na kudai kutokana na shida za vibarua ndiyo maana wamekuwa wakivumilia unyanyasaji huo.

“Amekuwa akitutukana matusi na kuwafikisha polisi baadhi ya wafanya kazi akidai ni wezi bila kosa lolote na kwamba anajidai kuwa yeye yu pamoja na viongozi wakubwa hivyo hakuna watakachokifanya juu yake” alisema mmoja wa wafanyakazi wa shirika hilo.

“Tunaomba mtufikishie malalamiko yetu kwa viongozi wa juu ili watambue kwamba sisi watanzania bado ni watumwa licha ya kuwa kuwa tuko kwenye nchi yetu na mtu mmoja tu Badri Dart” alisema mfanyakazi mwingine.

“Ikiwa huyu kiongozi ataondoka ni ukweli kwamba hili shirika litatengamaa ndani na nje ya shirika hili maana hata wananchi wanamlalamikia yeye tu.aliongeza mfanya kazi mwingine.

Hata hivyo kiongozi huyo ambaye aliwahi kufanya kazi katika Hoteli ya kitalii ya Sea Cliff iliyopo jijini Dar es salaam alikana shutuma hizo kwa kudai kuwa ni za uongo.

Baada ya JAIZMELA kuongea na Badri Darti alisema kuwa yeye amekuwa akifuata sheria za shirika na kwamba yeye ni mfuatiliaji makini wa mambo ya kampuni na kudai kuwa hiyo inaweza kuwa sababu moja ya kuchukiwa na wafanyakazi na hata wananchi wa nje.

Hata hivyo Badri alikiri kuwafikisha baadhi ya wafanya kazi katika vyombo vya sheria kwa madai ya wizi ingawa alisema kuna wengine kesi zao walishinda na wengine shirika lilishinda huku akisema wengine zinaishia juju tu.

“Asili ya watu wa kapunga ni wezi ingawa wengine wanatushinda kesi na wengine tumeshinda kesi mahakamani ila wengine kesi zao zinaishia juju tu” alisema Badri.

Akizungumzia kutumia uhusiano wake na viongozi wakubwa kuwanyanyasa wananchi pamoja na wafanyakazi wake alisema hiyo si kweli isipokuwa viongozi wameomba mashamba katika shirika lao na kudai wapo pale kama watu wakawaida na si kama mtumishi wa serikali hiyo hizo shutuma ni za uzushi.

Hata hivyo alikiri kuwepo viongozi wakubwa katika mashamba hayo akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Jaji Mkuu wa Mkoa Maafisa wa TRA pamoja na Askari 6 ambao wamepewa mashamba katika shirika hilo.

Awali alikana kuwepo na uhusiano wa karibu na kiongozi aliyetajwa kwa jina la Maheshi Patel lakini baada ya kubanwa na maswali alikiri kuwepo na uhusiano na mtu huyo na kudai kuwa ni rafiki yake na baadaye kuwa ni Bwana shamba.

Hata hivyo uchunguzi uliofanywa na JAIZMELA umebaini kuwa Maheshi Patel ndiye mwekezaji wa shamba la Kapunga na humtumia Badri dart kama “Technician” pia kama mkaguzi wa ndani wa shirika na utawala.
Posted by JAIZMELA at 14:41 0 comments

Saturday, April 10, 2010

HABARI ZA PASAKA

Na Godfrey Msomba
MIJO


SIKU zote mwanadamu huhitaji kupumzika ili siku inayofuata aweze kufanya vizuri zaidi ya jana hivyo naamini hata wewe umepumzika vya kutosha ili ufanye leo vizuri

KWA LEO INATOSHA.

Monday, March 15, 2010

KUNANI LEO MIAKA ILIYOPITA

Na Johnson Jabir
MIJO, MBEYA


Siku kama ya leo miaka 156 iliyopita, inayosadifiana na tarehe 15 Machi 1854 Miladia, alizaliwa Emil Adolf von Behring tabibu mashuhuri wa Ujerumani. Baada ya kumaliza masomo yake, Behring aliendeleza utafiti wa Louis Pasteur mwanakemia wa Kifaransa katika uwanja wa kuvumbua na kuzuia kuibuka maradhi ya kuambukiza. Kutokana na juhudi zake hizo, mnamo mwaka 1901 kwa mara ya kwanza kabisa alitunukiwa tuzo ya Nobel kwa upande wa tiba. Emil Adolf von Behring alifariki dunia mwaka 1917.
Siku kama ya leo miaka 30 iliyopita inayosadifiana na 24 Esfand 1358 Hijria Shamsia, ulifanyika uchaguzi wa kwanza wa bunge hapa nchini baada ya ushindi wa mapinduzi ya Kiislamu. Uchaguzi huo ulikata kiu kabisa cha wananchi wa Iran kwa miaka kadhaa ambao waliweza kupiga kura zao kwa uhuru na kuwachagua wabunge wawatakao. Uchaguzi huo ulifanyika huku kukiwa na njama kadhaa za maadui wa Kiislamu ambao walikuwa hawataki kuona demokrasia hiyo ikithibiti hapa nchini.

Siku kama ya leo miaka 25 iliyopita, inayosadifiana na 24 Esfand 1363 vibaraka wanaofungamana na madola ya kibeberu ya magharibi, walitega na kulipua bomu kwenye mkusanyiko mkubwa wa waumini wa sala ya Ijumaa mjini Tehran na kupelekea watu kadhaa kuuawa shahidi na wengine kujeruhiwa. Jambo la kuzingatiwa hapa ni kuwa, mlipuko huo wa sala ya Ijumaa haukusababisha hata kidogo kusimamishwa ibada hiyo, kwani Ayatullah Khamenei aliyekuwa khatibu na Imamu wa sala ya Ijumaa kwa siku hiyo aliendeleza shughuli za ibada hiyo kwa utulivu mkubwa.

Siku kama ya leo miaka 21 iliyopita, inayosadifiana na 15 Machi 1989, ardhi za Taba zilizoko kaskazini mashariki mwa Misri, zilikombolewa baada ya kukaliwa kwa mabavu na utawala wa Kizayuni wa Israel kwa miaka kadhaa. Utawala wa Kizayuni wa Israel ulilikalia kwa mabavu eneo la Taba lililoko upande wa mashariki mwa jangwa la Sinai, wakati wa vita vya mwaka 1967. Hatimaye jangwa la Sinai lilirejeshwa kwenye ardhi ya Misri baada ya kutiwa saini makubaliano ya Camp David kati ya Misri na Israel mwaka 1987

Friday, March 12, 2010

SOMO:NEWS WRITING

Na Johnson Jabir
MIJO, MBEYA


Mwanachuo mwenzangu ni vizuri kusoma na hili ili liweze kukusaidia katika somo hili la "NEWS WRITING".

News style (also journalistic style or news writing style) is the prose style used for news reporting in media such as newspapers, radio and television. News style encompasses not only vocabulary and sentence structure, but also the way in which stories present the information in terms of relative importance, tone, and intended audience.

News writing attempts to answer all the basic questions about any particular event - who, what, when, where and why (the Five Ws) and also often how - at the opening of the article. This form of structure is sometimes called the "inverted pyramid," to refer to the decreasing importance of information in subsequent paragraphs.

News stories also contain at least one of the following important characteristics relative to the intended audience: proximity, prominence, timeliness, human interest, oddity, or consequence.

MAADILI KATIKA UANDISHI WA HABARI


Accuracy and standards for factual reporting
Reporters are expected to be as accurate as possible given the time allotted to story preparation and the space available, and to seek reliable sources.
Events with a single eyewitness are reported with attribution. Events with two or more independent eyewitnesses may be reported as fact. Controversial facts are reported with of the publisher is desirable
Corrections are published when errors are discovered
Defendants at trial are treated only as having "allegedly" committed crimes, until conviction, when their crimes are generally reported as fact (unless, that is, there is serious controversy about wrongful conviction).
Opinion surveys and statistical information deserve special treatment to communicate in precise terms any conclusions, to contextualize the results, and to specify accuracy, including estimated error and methodological criticism or flaws.
Slander and libel considerations

Reporting the truth is almost never libel[7], which makes accuracy very important.
Private persons have privacy rights that must be balanced against the public interest in reporting information about them. Public figures have fewer privacy rights in U.S. law, where reporters are immune from a civil case if they have reported without malice. In Canada, there is no such immunity; reports on public figures must be backed by facts.
Publishers vigorously defend libel lawsuits filed against their reporters, usually covered by libel insurance.
Harm limitation principle

During the normal course of an assignment a reporter might go about—gathering facts and details, conducting interviews, doing research, background checks, taking photos, video taping, recording sound -- harm limitation deals with the questions of whether everything learned should be reported and, if so, how. This principle of limitation means that some weight needs to be given to the negative consequences of full disclosure, creating a practical and ethical dilemma. The Society of Professional Journalists' code of ethics offers the following advice, which is representative of the practical ideals of most professional journalists. Quoting directly:[17]

Show compassion for those who may be affected adversely by news coverage. Use special sensitivity when dealing with children and inexperienced sources or subjects.
Be sensitive when seeking or using interviews or photographs of those affected by tragedy or grief.
Recognize that gathering and reporting information may cause harm or discomfort. Pursuit of the news is not a license for arrogance.
Recognize that private people have a greater right to control information about themselves than do public officials and others who seek power, influence or attention. Only an overriding public need can justify intrusion into anyone's privacy.
Show good taste. Avoid pandering to lurid curiosity.
Be cautious about identifying juvenile suspects or victims of sex crimes.
Be judicious about naming criminal suspects before the formal filing of charges.
Balance a criminal suspect's fair trial rights with the public's right to be informed

UFIKAPO MBEYA ANGALI HII

Thursday, March 11, 2010

MUDA SIO RAFIKI YETU

Na Johnson Jabir
SOMIJO, MBEYA


Siku zote kila kitu huanza kama mchicha, pia hakuna marefu yasiyokuwa na ncha
Hivyo kila kitu ukifanyacho dhamiria kuweka alama au ukumbusho katika dunia hii ambayo ina mwisho na wewe kama mwanadamu una mwisho

Kumbuka Muda sio rafiki wa mwanadamu hususani Mjasirialimali kama mimi na wewe.

MAMBO NDIYO YAMEANZA